• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WITO WATOLEWA WANAWAKE KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI ZILIZOPO.

Posted on: March 6th, 2023


WITO WATOLEWA WANAWAKE KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI ZILIZOPO.



Wito watolewa kwa Wanawake wa Mkoa wa Songwe kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo katika maeneo yao ili wajiinue kiuchumi na kuondokana na ukatili ambao wamekuwa wakifanyiwa kutokana na kukosa nguvu ya uchumi.



Ushauri huo umetolewa na  Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe, Bi. Happiness Seneda wakati wa Kongamano la Wanawake ambalo limefanyika Machi 6 ikiwa ni kuelekea kilele cha siku ya wanawake Duniani Machi 8 ambalo kwa Mkoa wa Songwe litafanyika Wilaya ya Mbozi.



Bi. Happiness Seneda ametoa wito kwa wanawake kujitahidi kujiinua kiuchumi kwasababu wanawake waliowengi wanafanyiwa vitendo vya ukatili kutokana na kukosa nguvu ya kiuchumi na kumtegemea mwanaume tu.



Wanawake tuchangamkie fursa ya mikopo ya 10% ambayo inatolewa kwenye kila Halmashauri kwani fedha zipo na kwa mwaka wa fedha uliopita Halmashauri zimeweza kutoa zaidi ya Bilioni 1.2 ya 10% za mapato ya ndani hii yote ni fursa kwa wanawake, amesisitiza, Katibu Tawala, Bi. Happiness Seneda.



"Wanawake tujitahidi kuimarisha uchumi wetu uwe imara, kwani ukiwa na uchumi imara huwezi kufanyiwa ukatili, hivyo tuchangamkie fursa zilizopo kwenye maeneo yetu" Bi. Happiness Seneda.



Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Esther Mahawe ametoa wito kwa wanawake kuwa wajasili, kujianini na kuthubutu katika kuanzisha Biashara mbalimbali za kujikomboa kiuchumi.



Mhe. Esther Mahawe amewasihi wanawake kuachana na kauli ya "wanawake wakiwezeshwa wanaweza" badala yake wachangamkie wao fursa mbalimbali za ufugaji, Kilimo na Biashara ili wawe na nguvu ya kiuchumi.



Mfano kwa sasa ni Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uongozi wake amefanya mambo makubwa kiasi cha wanaume nao wanashangaa ambayo yanaonyesha kwa dhati kuwa mwanamke anaweza bila kuwezeshwa.



"Hakuna kilichosimama miradi mikubwa inaendelea, miradi mikubwa inaanzishwa, watoto wetu sasa wanasoma bila ada kuanzia awali hadi kidato cha sita, miundombinu inaboreshwa na wazazi saizi inapofika Januari hawakimbizani na ada" Mhe. Esther Mahawe.



Mhe. Mahawe ametoa wito kwa wanawake kuachana  na tabia ya kusubiria Baba alete kila kitu nyumbani kwani izo enzi sasa zimepita enzi za sasa ni Baba na Mama wote wanaleta nyumbani.



Wanawake msiogope kuanguka kwenye Biashara ata ukianguka mara mia inuka anza tena, ni bora uanze ufeli lakini ukiogopa kuanza huwezi kufanikiwa, amesisitiza Mhe. Mahawe.



Wakati huo huo, Katibu Tawala, Bi. Happiness Seneda ametoa wito kwa wanawake kuhakikisha wanawatunza watoto wao dhidi wa watu wenye nia ovu ya kuwafanyia ukatili  wakati wanapambana na kutafuta fursa za kiuchumi.



MWISHO.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.