• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

THPS YABORESHA HUDUMA ZA KIFUA KIKUU MIKOA YA SONGWE, KATAVI, RUKWA NA KIGOMA.

Posted on: August 4th, 2021

 THPS YABORESHA HUDUMA ZA KIFUA KIKUU MIKOA YA SONGWE, KATAVI, RUKWA NA KIGOMA.

SONGWE: Tanzania ni miongoni mwa Nchi 30 zinazochangia 87% ya wagonjwa wa kifua kikuu Duniani na inakadiriwa kuwa kati ya watu 100,000 watu 237 wanaugua kifua kikuu kila mwaka Tanzania na kwa mujibu repoti ya shirika la Afya Duniani (WHO) ya 2020 Tanzania inakadiriwa kuwa na wagonjwa 137,000 waliogua kifua kikuu na 2019 waligundulika wagonjwa 81,208 ikiwa ni ongezeko la 5,363 kutoka 78,845 ya waliogundulika 2018 ambayo ni sawa na 59% na hivyo kuwa na takribani 41% ya watu ambao wanamaambukizi ya kifua kikuu lakini hawajatambulika Tanzania.

Kwa sababu hiyo, Shirika la Tanzania Health Promotion Support (THPS) limeboresha huduma ya tiba ya kifua kikuu kwa Mikoa ya Kigoma, Katavi, Rukwa na Songwe kwa kuwakabidhi vifaa tiba vya vya kuchunguza ugonjwa wa kifua kikuu vya thamani ya Milioni 420 ambavyo vimekabidhiwa Mkoa wa Songwe kwa niaba ya Mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma.

Muwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Songwe ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Cosmas Nshenye amepokea vifaa hivyo kwa niaba ya Mikoa hiyo katika hafla iliyofanyika katika Zahanati ya Mlowo Wilaya ya Mbozi leo Agosti 4.

Vifaa vilivyotolewa na THSP ni Mashine za Genaexpert 8 za kutambua Kifua kikuu ambayo moja inauzwa Milioni 44 kila Mkoa utapata mashine 2 gharama ya mashine ni Milioni 355 pamoja na Hadubini (Led microscope)11 kila moja in Milioni 5.9 sawa na Milioni 65 jumal ya vifaa vyote ni thamani ya Milioni 420.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Missaile Musa amewataka watumishi wa Afya kuvitunza vifaa hivyo kwani vifaa vikitokewa na wadau Kwa Serikali vinakuwa ni mali ya Serikali na vinatakiwa kutunzwa vizuri na kuwahudumia wananchi kwa ufasaha.

George Musyani, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mbozi, ni miongoni mwa wananchi ambaye ameuguza ndugu yake kwa muda mrefu bila kugundua kama ana kifua kikuu kwa sababu ya Kukosekana kwa vifaa tiba ambayo vinaweza kugundua kifua kikuu hadi pale alipoenda Mkoa wa Mbeya na kubaini ndugu yake ana kifua kikuu, hivyo amewashukuru wadau kwa kufanikisha vifaa vya Genaexpert kwa Mkoa wa Songwe kwani vitakwenda kusaidia kugundua matatizo ya kiafay kwa wananchi haswa wale wenye kifua kikuu kilichojificha.

"Mwaka 2019 Mkoa wa Songwe ulikuwa na mgonjwa mmoja sugu wa kifua kikuu lakini 2020 walipatikana wagonjwa 6 sugu na hii ni hatarii wanapokuwa kwenye jamii bila kugundulika, hivyo ni matarajio yangu vifaa hivi vitakwenda kufanya kazi ya kuwagundu wagonjwa wa kifua kikuu mapema na kwa Haraka" Cosmas Nshenye Mkuu wa Wilaya ya Mbozi.

Mkoa wa Songwe 2020 ulifanikiwa kugundua wagonjwa 715 wa kifua kikuu sawa 83%, Hii inaonyesha Mkoa bado unawagonjwa wa kifua kikuu lakini bado hawajatambuliwa na kusababisha kuambukiza watu wengine.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA MOMBA KUJADILI HOJA ZA CAG

    June 11, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI HOJA ZILIZO BAINISHWA KATIKA RIPOTI YA CAG HALMASHAURI YA MBOZI

    June 10, 2025
  • RC CHONGOLO APIONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE KWA KUPATA HATI SAFI

    June 10, 2025
  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.