• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WASICHANA ELFU 20 KUPATIWA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI SONGWE

Posted on: April 16th, 2018

Takribani Wasichana 20,900 wenye umri wa miaka 14 wanatarajia kupata chanjo ya kuwakinga dhidi ya ugonjwa wa saratani ya Mlango wa kizazi Mkoani Songwe kuanzia Aprili 23 Mwaka huu.
Chanjo hiyo inatolewa kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 kwa mara ya kwanza na dozi ya pili watapewa miezi sita baadaye ili kukamilisha kinga dhidi ya saratani hiyo.
Akizindua chanjo hiyo katika shule ya Sekondari ya Vwawa Wilaya ya Mbozi Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa amesema chanjo hiyo ni juhudi za serikali za kuboresha na kuokoa maisha ya wananchi hasa kwa magonjwa yanayozuilika.
Gallawa ameeleza kuwa chanjo hiyo ni salama na imethibishwa na shirika la Afya duniani na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania hivyo wazazi na walezi washirikiane na serikali kuhakikisha wasichana hao wanapata kinga hiyo.
“Kinga ni bora kuliko tiba, tukishirikiana vyema wazazi na serikali tutaweza kuokoa maisha ya mabinti zetu, ugonjwa huo wa saratani ya mlango wa kizazi inaongoza kwa vifo vya akina mama vitokanavyo na saratani nchini kwetu”, amesisitiza.
Aidha amewasihi wasichana wote kutoshiriki vitendo vya ngono katika umri mdogo kwakuwa ni moja ya chanzo kinachoweza kusababisha saratani ya mlango wa kizazi pamoja ikiwa ni pamoja na kutojiingiza katika uvutaji wa sigara.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt Kheri Kagya amesema chanjo hii inatolewa bure katika vituo vyote vya kutolea huduma za Afya na katika huduma za mkoba kwenye shule mbalimbali.
Dkt. Kagya ameongeza kuwa chanjo hii itakuwa endelevu huku akibainisha kuwa takwimu zinaonyesha kila mwaka akina mama elfu 50 wanapata saratani hii na asilimia 58 ya wanaopata ugonjwa huo hufariki.
Naye Atuganile Shimwela mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari ya Vwawa ameeleza kuwa amefurahi kupatiwa chanjo ya kumkinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi.
“Nimefurahi kwakuwa sasa niko salama dhidi ya saratani hiyo na nitawashauri wenzangu pia wapate chanjo hiyo, pia tutafuata ushauri wa mkuu wetu wa mkoa wa kutojiingiza katika ngono katika umri wetu mdogo ili tuispate magonjwa”, ameeleza. .

Wanafunzi wa Sekondari ya Vwawa Wilaya ya Mbozi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa wakati wa uzinduzi wa Chanjo ya Saratani ya Mlango wa Kizazi mapema jana.

Matangazo

  • ILEJE DC WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • MBOZI DC WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • MOMBA DC WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • SONGWE DC WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Dkt. SHEKALAGHE VYUO VYA UFUNDI NA VIKUNDI VYA UJASILIAMALI MBADALA KWA WANAFUNZI AMBAO HAWAJAFAULU

    December 18, 2020
  • Dkt. SHEKALAGHE AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA PESA YA UJENZI WA MADARASA KILA MWAKA.

    December 18, 2020
  • SONGWE: WANANCHI WAHIMIZWA KUPIMA UKIMWI KUJUA HALI ZAO KUEPUKA MAAMBUKIZI MAPYA

    December 01, 2020
  • RC MWANGELA AWATAKA WAFANYABIASHARA KUUZA BIDHAA KWA BEI ELEKEZI

    November 28, 2020
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Boma Road, Vwawa, Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras.songwe@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.