• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIFUGO

SEKTA YA MIFUGO

Idadi ya Mifugo.

Sekta ya Mifugo ni mojawapo ya shughuli kuu za kiuchumi inayotegemewa na wananchi wa Mkoa wa Songwe. Mkoa unajitosheleza kwa mahitaji ya nyama na kiasi kikubwa cha mifugo husafirishwa kwenda nje ya mkoa.

 

JEDWALI NA: IDADI YA MIFUGO NDANI YA MKOA.

Mnyama

Halmashauri

Jumla
 
Ileje
Mbozi
Momba
Tunduma
Songwe
Ng’ombe asili

39602

107681

11,8027

5265

123,756

394,331

Ng’ombe maziwa

3392

6752

401

92

105

10742

Mbuzi

32545

61,781

73,497

615

72,955

241,393

Kondoo

3,757

5,256

9,884

97

13,305

32,299

Nguruwe

6396

23,343

8067

2332

33,046

73,184

Kuku asili

148,809

560,925

155,233

39289

153,695

1,057,951

Kuku kisasa

571

2,550

10,351

9136

-

22,608

Bata

-

3,860

5,096

216

-

9,172

Punda

16

722

1,547

39

1,174

3,498

Chanzo: Halmashauri za Wilaya, 2017

 

BORESHAJI WA MIFUGO.

Mkoa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa ufugaji umeendelea kuboresha mifugo ili kuongeza uzalishaji wenye tija hasa kwa ng’ombe wa maziwa, kuku pamoja na nguruwe. Mifugo hii imekuwa ikinunuliwa kupitia miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na ASDP/DADPS, ACGG na Heifer International ambapo Mradi wa Heifer umenunua ng’ombe 200 kwa wafugaji wa kata za Isansa na Igamba katika Wilaya ya Mbozi na wamesambazwa kwa wafugaji.

MAGONJWA YA MIFUGO.

Mkoa unakumbwa na magonjwa yanayoenezwa na kupe, chambavu, kuharisha, mapere ngozi, kichaa cha mbwa, minyoo, ukurutu na homa ya nguruwe.

KUTENGA MAENEO.

Eneo lililotengwa kwa ajili ya mifugo ni hekta 261,516.18  kwa ajili ya malisho katika Wilaya za Momba na Songwe. Katika Wilaya ya Momba vijiji vilivyotenga maeneo ya malisho ni 20 na Songwe ni vijiji 8

HALI YA UTAMBUZI, USAJILI NA UFUATILIAJI WA MIFUGO.

Zoezi la Utambuzi na Usajili kwa kupiga chapa katika Mkoa lilichelewa kuanza kutokana na ufinyu wa bajeti ambapo ilipelekea hali ya uhamasishaji kuchukua muda mrefu. Zoezi limeanza mwezi Oktoba ambapo lilizinduliwa Rasmi tarehe 17 Oktoba 2017 na Mhe. Mkuu wa Mkoa katika Wilaya ya Songwe. Hadi kufikia tarehe 02 Disemba 2017 Jumla ya ng’ombe 94991 (Ileje 18282,  Mbozi 43779, Songwe 28,173 na Tunduma 4757) wamepigwa chapa .

Uhimilishaji

Mkoa wa Songwe uhimilishaji unaendelea katika Halmashauri ya Mbozi. Ng’ombe 474 wamehilimishwa kipindi cha Januari 2017 - Septemba 2017 kati ya lengo la ng’ombe 500 kwa mwaka.

UZALISHAJI MAZAO YA MIFUGO

Nyama

Mkoa umezalisha kilo za nyama 2,326,832 katika kipindi cha Januari 2017 – Septemba 2017.  


Maziwa

Jumla ya lita 14,136,400  zenye thamani ya Sh. 9,895,480,000 zimezalishwa kwa kipindi cha januari 2017  mpaka Septemba 2017 kwa ujumla kutoka ng’ombe wa aina zote na mbuzi.

 

Ngozi

Uzalishaji wa ngozi ni wa shida kutokana na kutokuwepo kwa bei nzuri na soko la uhakika. Kipindi cha Januari 2017 - Septemba 2017 vipande vya ngozi  9,740 vya ng’ombe, vipande 7,842 vya mbuzi na kondoo vipande 3,694 vilikusanywa.

Mauzo ya Mifugo 

Mkoa una jumla ya minada 7 inayofanya kazi katika Halmashauri za Wilaya Ileje, Mbozi, Momba na Songwe. Kipindi cha Julai 2017 - September 2017 jumla ya ng’ombe 2,854 wenye thamani ya Sh. 1,926,450,000. waliuzwa, mbuzi na kondoo 2,461 wenye thamani ya Sh. 147,660,000.00 waliuzwa.

Miundo mbinu ya mifugo

Malambo

Mkoa una lambo moja katika kijiji cha Kasanu Wilaya ya Momba kwa ajili ya kunyweshea mifugo. Ujenzi wa lambo katika kijiji cha Mkomba Wilaya ya Momba unaendelea na ujenzi wa bwawa la Mbangala katika Wilaya ya Songwe unaendelea na linajengwa na Wakala wa Mabwawa na Visima (DDCA) kwa fedha za Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa gharama ya Sh. 2,400,000,000.00

Machinjio  na makaro

Mkoa una machinjio makubwa 8 na makaro 37. Machinjio na makaro haya yanatumika katika kuchinjia ng’ombe, mbuzi kondoo na nguruwe. Ambapo ng’ombe, mbuzi na Kondoo hutumia kwa pamoja isipokuwa machinjio ya nguruwe hujitegemea.

Jedwali. Na. 17 Machinjio yaliyopo katika Mkoa wa Songwe

Halmashauri 
Mbozi
Momba 
Ileje
Tunduma
Songwe
Jumla 
Machinjio

2

1

2

1

2

8

Makaro

10

8

4

2

13

37

 

Hali ya majosho

Mkoa una majosho 7 kati ya hayo 2 ni mazima na yanafanya kazi, Majosho 5 hayafanyi kazi kwa sababu ya ukosefu wa maji, kuingiliwa na wakulima kwa kulima kwenye njia za kwenda kwenye majosho na ujenzi wa makazi. Mkakati wa kukabiliana na hali hiyo umewekwa kwa kusisitiza na kuhimiza wafugaji kuogesha kwa kunyunyizia na zaidi kuzingatia chanjo ya ndigana kali.

 

Miundombinu mingine

Mkoa katika Wilaya ya Mbozi ina mitambo ya Biogas 127 na kati ya hiyo  mitambo 117 inafanya kazi.

Afya ya mifugo

Mkoa una vituo viwili vya kutolea huduma za mifugo (LDC’s), kimoja kipo Halmashauri ya Ileje na kingine Halmashauri ya Mbozi. Sehemu kubwa ya huduma hutolewa katika maeneo ya wafugaji pale wataalam wanapowatembelea au kuitwa na wafugaji.

Magonjwa ya mifugo na matibabu yake

Magonjwa ya Mifugo yanayojitokeza sana katika Mkoa wa Songwe ni  magonjwa yanayoenezwa na kupe, chambavu, kuharisha, mapere ngozi, kichaa cha mbwa, minyoo, ukurutu na homa ya nguruwe. Magonjwa ya kuku ni mdondo, homa za matumbo na ndui

 

Maduka ya nyama

Mkoa una maduka ya nyama  84 katika Halmashauri zake tano.

 

Maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mifugo

Eneo lililotengwa kwa ajili ya mifugo ni hekta 261,516.18  kwa ajili ya malisho katika Wilaya za Momba na Songwe. Katika Wilaya ya Momba vijiji vilivyotenga maeneo ya malisho ni 20 Songwe ni vijiji 8.

Miradi ya mifugo

Miradi ambayo inaendesha shughuli za kuwasaidia wafugaji katika Mkoa wa Songwe ni Heifer International (T), East Africa Dairy Development II na East Africa Dairy Genetic Gain. Miradi hii inasaidia kuinua sekta ya Mifugo

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.