• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA SONGWE YAWAPONGEZA VIONGOZI WA SERIKALI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: January 23rd, 2024

Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) Mkoa wa Songwe imewapongeza viongozi wa Serikali Ngazi ya Mkoa na Halmashauri, Chama na taasisi za Serikali na ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Songwe kwa usimamizi na utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo.

Pongezi hizo zimetolewa, Januari 22, 2023 na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Ndugu Radwel Mwampashi wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Songwe ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa baadhi ya miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Songwe.


Akitoa majumuisho ya ziara hiyo, Ndugu Mwampashi amesema  kuwa miradi waliyoitembelea katika ziara ya sasa imekuwa na mabadiliko makubwa sana.

"Miradi ya safari hii imekuwa na mabadiliko makubwa sana katika Wilaya ya Songwe kwa kweli kwa niaba ya kamati ya siasa nawapa 'big up'. Nawapongeza sana. Hakuna mradi ambao umekuwa na kasoro na siku zote Wilaya ya Songwe imekuwa roal modal ya Mkoa wa Songwe. Hongereni sana" amesema Mwenyekiti huyo wa CCM Mkoa wa Songwe na kuongeza;


"Mimi kwa niaba ya kamati niwapongeze sana viongozi wa Wilaya ya Songwe. Kazi mnayoifanya ni nzuri lakini pia mambo   yanayofanyika mazuri kama haya ni juhudi za mheshimiwa Rais wetu ambaye usiku na mchana halali usingizi kuhakikisha wananchi wanapata huduma"


Pia, amewasisitiza viongozi wa Wilaya hiyo kushirikiana na kuombeana ili Mkoa huo uwe namba moja katika kusimamia na kutekeleza Ilani ya CCM pamoja na kujipanga kuelekea kwenye chaguzi zijazo.


kamati ya Siasa, pia iliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Dkt. Francis K. Michael,  Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Happiness Seneda, wataalamu kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa, wametembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo mradi wa umeme wa REA katika Kijiji cha Itindi wenye thamani ya Sh359.7 milioni, ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Sambila yenye thamani ya Sh583 milioni na Shule mpya ya msingi ya Kikuyuni yenye thamani ya Sh538.5 milioni ya mradi wa BOOST.


Miradi mingine ambayo kamati hiyo imeitembelea na kuikagua ni pamoja na mradi wa barabara ya Chang'ombe-Patamela-Makongolosi wenye thamani ya zaidi ya Sh4 bilioni na mradi wa ujenzi wa barabara ya Shanta Ndogo-Njelenje ambao unatekelezwa kwa Sh584 milioni.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.