• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KIKAO KAZI NA KUKARIBISHA MRADI WA UMEME JUA SONGWE

Posted on: August 18th, 2017

KIKAO KAZI NA KUKARIBISHA MRADI WA  UMEME JUA

 

Mkuu wa Mkoa wa Songwe alifungua kikao kazi cha umeme jua ambacho kilihusisha Mwekezaji  Baraka Solar, Wataalam wa Sekretariet ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi Watendaji na Wenyeviti wa halmashauri wa Wilaya na Mji wa Tunduma katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi tarehe 10 Agosti,2017

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa aliwataka Washiriki kusikiliza kwa umakini maelezo ya mwekezaji kampuni ya Baraka Solar Specialists Ltd inayojishughulisha na usambazaji, uuzaji na ufungaji wa umeme Jua katika huduma za Jamii, hufunga pampu za kuvutia maji kwa kutumia nguvu ya jua ili kurahisisha upatikanaji wa maji vijijini na asilimia 80 ya miradi hufanywa kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya na Miji Tanzania. Aliongeza kuwa Kampuni ya Baraka Solar imekusudia kuwafikia Wananchi ambao wapo mbali na mpango wa Mradi wa Umeme Vijijini wa REA.

Baada ya ufunguzi huo, Mkuu wa Mkoa aliongea na Washiriki akianzia na  hatua ya Mkoa kuhamia kwenye matumizi ya TEHAMA ambapo alizitaka kila Halmashauri kufanya mafunzo ya matumizi ya Tablets ya awali wakati wanasubiria mafunzo ya baadaye ambayo yatahusisha mfumo ambao utawezesha Vifaa hivyo kufanya kazi ya kusambaza, kutunza nyaraka kwa njia ya usalama na ufanisi na siyo kufanya kazi nyingine.

Pia alisisitiza kuwa kila Halmashauri kufanya vikao vya Pembejeo mapema kabla ya msimu wa Kilimo kuanza, alisema ni vizuri kujua pembejeo gani zinahitajika katika Halmashauri kwa kuzingatia maeneo ya kijiografia.

Ili kuhakikisha kuwa Mkoa unapata pembejeo zenye  viwango vinavyotakiwa Mkuu wa Mkoa aliagiza kuwa vikao hivyo vihusishe wadau wote wa Pembejeo kwa mfano vyama vya Wakulima, Wasambaza pembejeo n.k. aliagiza kuwa wasambazaji watume maombi ya kuonesha nia ya kusambaza pembejeo na kupata nafasi ya kujieleza watakavyoweza kusambaza pembejeo hizo kwa kuzingatia mikataba itakayoandaliwa na  Wanasheria wa serikali.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa kwa kutumia njia hiyo itakuwa rahisi kulinda ubora wa pembejeo na kumfikia mtumiaji kwa wakati pia msambazaji wa pembejeo feki atajulikana kwa urahisi na sheria zitachukua mkondo wake.

Vilevile aliagiza kuwa uendeshaji wa vikao vya Pembejeo wa awali uliohusisha mgao wa pembejeo za ruzuku ubadilike na kuwa na mtizamo mpana zaidi kwa kushirisha Maafisa Kilimo, Maendeleo ya Jamii, Biashara ili wakulima na Halmashauri waweze kunufaika na kuziba mianya ya pembejeo feki katika Mkoa wa Songwe.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.