• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KITENGO CHA MANUNUZI NA FEDHA MTEGONI UKAMILISHAJI WA MIRADI YA AFYAMBOZI:

Posted on: June 4th, 2022

KITENGO CHA MANUNUZI NA FEDHA MTEGONI UKAMILISHAJI WA MIRADI YA AFYAMBOZI:

Kusuasua kukamilika kwa miradi ya Afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kumewaweka mtegoni watumishi wa Kitengo cha fedha na manunuzi.Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba amesema ifikapo 30 Juni 2022 kama Kituo cha Afya Hezya, Nambinzo na Halungu vitakuwa havijakamilika watumishi wa kitengo cha Manunuzi na Fedha watapaswa kujitathimini kama wanatosha kwenda na kasi ya Rais Samia Suluh Hassan ndani ya Mbozi na Mkoa wa Songwe.Mkuu wa Mkoa wa Songwe ametoa kauli hiyo wakati akifanya ukaguzi wa miradi ya Afya katika Kituo cha Afya Hezya, Nambinzo na Halungu na kukutana na baadhi ya wajumbe wa Kamati za ujenzi pamoja na wananchi wakilalamika dhidi ya utendaji wa kazi wa Kitengo cha Manunuzi na Fedha kinachopelekea kuchelewa kwa baadhi ya manunuzi."Nimeenda Kituo cha Afya Hezya nimekuta wanalalamikia Kitengo cha manunuzi na fedha na hapa Halungu nao wanalalamikia hivyo hivyo kwa kuchelewesha madokezo" Mhe. Omary Mgumba.Serikali imetoa fedha Milioni 500 ujenzi wa Kituo cha Afya Hezya, milioni 500 ujenzi wa kituo cha Afya Nambinzo milioni 500 fedha za mapato ya ndani ujenzi wa kituo cha Afya Halungu na Milioni 300 Kituo cha Afya Itaka.Elias Mboya mkazi wa Hezya na mjumbe wa Kamati ya manunuzi ameiomba Serikali ipunguze mlolongo wa kwenda na kurudi ili ujenzi ufanyike kwa haraka.Willy Mondya Diwani wa Hezya amesema tatizo lipo upande wa mdokezo kuchelewa kwa mtu kupitia zaidi ya sehemu 3 na ikitokea mtu mmoja hayupo basi dokezo linasimama na kazi zinasimama.Mawazo Tuyanje ameiomba Serikali kuweka utaratibu wa fedha za kuwalipa mafundi zisichukue zaidi ya wiki ili miradi ikamilike na mafundi wafanye kazi kwa bidii.Maarifa Mwashitete ambaye ni Diwani wa Kata ya Halungu ameiomba Serikali kufanya maboresho kwenye. Kitengo cha manunuzi ili wafanye kazi kwa kasi tofauti na sasa.Miradi ya Afya imekuwa inaenda kwa kusuasua licha ya Serikali kuleta fedha za miradi tangu 2021 tofauti na miradi ya Elimu ambayo inakwenda vizuri.MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA MOMBA KUJADILI HOJA ZA CAG

    June 11, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI HOJA ZILIZO BAINISHWA KATIKA RIPOTI YA CAG HALMASHAURI YA MBOZI

    June 10, 2025
  • RC CHONGOLO APIONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE KWA KUPATA HATI SAFI

    June 10, 2025
  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.