• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MACHIFU SONGWE KUSIMAMIA TIBA YA KUJIFUKIZA

Posted on: April 30th, 2020

Uongozi wa machifu Mkoani Songwe umeipongeza serikali kwa kutambua na kuruhusu matumizi ya Tiba za Asili kama vile kujifukiza huku ukiahidi kusimamia matumizi sahihi ya tiba hizo hususani katika kupambana na Ugonjwa wa Corona.

Mwenyekiti wa Machifu Mkoa wa Songwe Chifu Mbeshena Nzunda ameyasema hayo wakati alipokutana na Mkuu wa Mkoa wa Songwe kujadiliana namna bora ya kutumia njia za tiba za asili kama vile kujifukiza katika kutibu magonjwa ya mfumo wa upumuaji.

Chifu Nzunda amesema njia ya asili ya kujifukiza kwa kutumia miti, majani au mizizi wanaifahamu na imekua ikitoa nafuu kwa wagonjwa wa mafua na kikohozi huku akiwataka waganga wanaotoa tiba ya kufukiza wasitumie maji ya moto sana wala kufukiza muda mrefu kufukiza.

Amesema machifu wamekubaliana kufuata maelekezo ya serikali huku wakiwasimamia waganga wote na endapo watajitokeza watakaoenda kinyume na utaratibu wa serikali watawaripoti katika vyombo vya sheria pia wagonjwa wasijifukize nyumbani bali wawaone waganga wenye leseni ili wapate tiba sahihi.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela amewataka machifu kutumia uzoefu walio nao wa kufahamu mizizi, miti na majani yanayo weza kutibu magonjwa mbalimbali watoe tiba hizo bila kuweka masharti yasiyo faa kwa wananchi.

Brig. Jen. Mwangela amesema lengo la serikali ni kutaka shughuli ziendelee licha ya uwepo wa ugonjwa wa Corona pia wananchi wawe na afya njema hivyo tiba za asili zinazo weza kutoa nafuu kwa wagonjwa zinaruhusiwa kutumika.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt Hamad Nyembea amesema tiba za asili hususani njia ya kufukia imekuwa ikitumika katika mataifa mbalimbali na imekuwa ikitoa nafuu kwa wagonjwa wenye matatizo katika mfumo wa upumuaji.

Dkt Nyembea amesema njia ya kufukiza sio tiba kwa asilimia 100 bali hutoa usaidizi kwa mgonjwa wa matatizo ya njia ya hewa aweze kupumua vizuri na pia kujifukiza sio kinga ya ugonjwa wa Corona.

Amesema licha ya serikali kuendelea kutoa matibabu ya hospitali kwa magonjwa ya mfumo wa hewa kama mafua na kikohozi pia kuna umuhimu wa kutopuuzia tiba asili ya kujifukiza kwakuwa hutoa unafuu kwa mgonjwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.