• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIRADI YA "FORCE ACCOUNT" YAMFRAHISHA RC MICHAEL, ATOA PONGEZI KITENGO CHA MANUNUZI, FEDHA.

Posted on: May 14th, 2023

MIRADI YA "FORCE ACCOUNT" YAMFRAHISHA RC MICHAEL, ATOA PONGEZI KITENGO CHA MANUNUZI, FEDHA.

MOMBA: Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Dkt. Francis Michael ameupongeza uongozi wa Wilaya ya Momba pamoja na Halmashauri ya Momba kwa kusimamia vizuri miradi kwa kutumia "Force account"

Mhe. Dkt. Francis Michael amesema hayo baada ya kufanya ukaguzi wa miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Momba na kuona miradi inaendelea vizuri na thamani ya fedha kwenye miradi inaonekana.

Mhe. Dkt. Francis Michael amekagua mradi wa kimkakati wa ujenzi wa machinjio ya kisasa uliopo soko la kisasa la kakozi ambao unathamani ya shilingi Bilioni 2, ukamilishaji wa zahanati ya Nakawale wa kwa thamani ya milioni 50.

Pia, ujenzi wa wa shule mpya ya sekondari ya Ikana ya thamani ya milioni 470, jengo la utawala la Bilioni 2, ukamilishaji wa Nyumba ya Mkurugenzi milioni 150 na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya jengo la wodi ya wazazi milioni 500 miradi yote inaendelea vizuri na thamani ya fedha inaonekana.

Nimeona miradi yenu inaendelea vizuri, viwango vizuri, inaonyesha jinsi gani hapa Kitengo cha manunuzi na fedha wanafanya kazi vizuri, miradi inaenda kwa wakati, kwa kweli hongereni sana Momba, amesisitiza Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Dkt. Francis Michael.

Pia, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Dkt. Francis Michael amesema sehemu nyingi hapa nchini miradi inayotekelezwa kwa "Force account" inakuwa inakwamishwa na watalamu wa Manunuzi na Fedha lakini kwa hapa Momba naona ilo jambo halipo kazi inafanyika vizuri, sijasikia changamoto ya kukwamishwa vifaa, kazi nzuri kwa Mkurugenzi wa Halmashauri na timu yako.

Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi Halmashauri ya Wilaya ya Momba, Bi. Safina Shapwata amesema ushirikiano mkubwa wanaopata kutoka kwa Mkurugenzi wao, Bi. Regina Bieda ndio chachu ya wao kufanya vizuri kwa mambo mbalimbali

Kwa kweli tumefarijika sana Mkuu wa Mkoa kutambua na kuona tunafanya kazi nzuri, nasi tunamhaidi kuwa tutafanya kazi na hatutamuangusha, amesema Bi. Safina Shapwata.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI DATA CLEARK, CLINICIAN NA NURSE October 01, 2021
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS SENEDA AWATAKA MAAFISA AFYA KUJA NA MIKAKATI YA KUSIMAMIA TAKA NGUMU.

    June 01, 2023
  • MIRADI YA "FORCE ACCOUNT" YAMFRAHISHA RC MICHAEL, ATOA PONGEZI KITENGO CHA MANUNUZI, FEDHA.

    May 14, 2023
  • ZAHANATI YA NJELENJE KUANZA KUTOA HUDUMA

    May 18, 2023
  • BWAWA LA MUKO LA BILIONI 1.9 KUHUDUMIA WANANCHI 11,671, MIFUGO 3,430.

    May 18, 2023
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras.songwe@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.