• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSIZEMBEE MAFUNZO YA CORONA- RC MWANGELA

Posted on: March 11th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela amewataka wataalamu wa afya Zaidi ya 40 kutofanya uzembe katika kusikiliza na kutekeleza mafunzo wanayo patiwa ya utayari wa kupambana na magonjwa ya Dharura ya Corona na Ebola.

Brig. Jen. Mwangela ameyasema hayo mapema leo wakati alipo tembelea eneo la mafunzo ya kukabiliana na Ebola na Corona  yanayo endeshwa kwa muda wa siku tano na Wizara ya Afya kwa Kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO).

“Ninasisitiza mafunzo haya ni muhimu sana, Msifanye uzembe wowote katika kusikiliza au hata itakapo tokea mgonjwa japo hatuombei atokee, kwani kwa kufanya uzembe ni hatari na hakuna atakaye tusamehe kwa katika hilo.”, amesisitiza Brig. Jen. Mwangela.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa Mkoa wa Songwe hasa kwakuwa ni lango la SADC na kuna muingiliano Mkubwa wa watu katika Mpaka wa Tunduma, huku kukikwa tayari na Nchi mbili za SADC ambazo kuna washukiwa wa ugonjwa huo.

Brig. Jen. Mwangela amesema Nchi za Kongo na Afrika Kusini tayari kuna washukiwa wa Ugonjwa wa Corona ambapo nchi hizo zina muingiliano Mkubwa na nchi yetu hivyo mafunzo haya yatasaidia kuweka utayari kwa kuzuia ugonjwa huo usiingie nchini au kutoa matibabu endapo atatokea mgonjwa.

Mkufunzi wa Magonjwa ya Dharura Dkt Prosper Mashaka amesema wamewajengea utayari watoa huduma za afya ambao ni madaktari, wauguzi, wateknolojia wa dawa na maabara, watu wanao husika na mazishi ili waweze kukabiliana na ugonjwa wa corona kwakuwa Songwe ni mpakani.

Dkt Mashaka amesema matarajio ya wakufunzi hao ni kuwa timu hiyo itawezesha utoaji wa huduma ya kuzuia au kutibu endapo atatokea mgonjwa wa corona lakini pia waliopata mafunzo watatoa elimu kwa watoa huduma wengine ili kuunda timu kubwa zaidi ya wataalamu wenye ujuzi huo.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt Dunstan Ligasiwa amesema Mkoa wa Songwe umechukua tahadhari zote Muhimu za kukabiliana na ugonjwa Corona na Ebola ikiwa ni pamoja na kuzingatia maelekezo ya Wizara ya Afya.

Dkt Ligasiwa amesema halmashauri zote Mkoani Songwe zimeelekezwa kutenga vituo vya Afya vitakavyo shughulika na wagonjwa wa Corona endapo watatokea pia kutenga vyumba maalumu katika kila kituo cha kutolea huduma za Afya kwa ajili ya upimaji endapo atabainika mshukiwa wa ugonjwa huo.

Ameongeza kuwa Mkoa umekusanya vifaa tiba vyote muhimu kwa ajili ya kukabilina na Ugonjwa huo pia mawasiliano na Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kwa ajili ya kuomba dawa na vifaa tiba vingine muhimu yamefanyika.

Dkt Ligasiwa amesema katika eneo la Mpaka wa Tunduma kila mgeni anayeingia Nchini anapimwa endapo ana ugonjwa wa Corona au Ebola huku mafunzo kwa wataalamu wengine wa afya yakiendelea ili kuwa na timu kubwa ya kukabiliana na ugonjwa huo.

Naye Mteknolojia wa Dawa kutoka Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe Prosper Alex Mfutakamba amesema mafunzo ya utayari wa kukabiliana na magonjwa ya Corona na Ebola yatawasaidia watoa huduma za Afya kujikinga wao wenyewe kwanza na pia kuweza kutoa huduma kwa wengine kwa usahihi Zaidi.

Muuguzi kutoka Hospitali ya Mwambani Wilaya ya Songwe Sharifa Soroiya amesema baada ya mafunzo hayo watoa huduma hao wako tayari endapo atatokea mgonjwa wa Corona lakini pia wanaiomba serikali kuweka vitendea kazi vyote muhimu ili waweze kutoa huduma hizo kwa usahihi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.