• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MZEE AMBILIKILE MWANYALUKE PANJA ANAYESADIKIKA KUWA NA UMRI WA MIAKA 127 SONGWE

Posted on: May 20th, 2017

HISTORIA FUPI YA MZEE AMBILIKILE MWANYALUKE PANJA ANAYESADIKIKA KUWA NA UMRI WA MIAKA 127

Imeandaliwa na mwandishi wetu.

Mzee Ambilikile Mwanyaluke Panja anayesadikika kuwa na umri wa miaka 127 anaishi katika kitongoji cha Izyika, Kijiji cha Majengo kata ya Ihanda umbali wa takriban Kilometa moja magharibi ya  kituo cha mabasi cha Ihanda kilichopo barabara kuu inayotoka Afrika Kusini kwenda Cairo Misri.

Mzee Panja kutokana na hali ya afya yake inayotokana na umri mkubwa alionao bado ana kumbukumbu ya matukio makuu ya kwa mfano biashara ya utumwa iliyoratibiwa na Chifu Melele wa Tatu, vita vya maji maji, Vita ya kwanza na ya pili ya dunia ndani ya Kijiji cha Majengo.

Aidha, Mzee Ambilikile amepungukiwa uwezo wa kusikia kwani ahitaji sauti kubwa ili kuweza kusikia vizuri, anaweza kumtambua mtu kama atakuwa karibu naye. Mpaka sasa ni miaka mitatu mzee Panja anatumia kiti cha magurudumu  kwa sababu hawezi kutembea kwa miguu yake.

Mzee huyo anapenda kutumia lugha yake ya asili ya Kindali  ingawa anasikia Kiswahili.

Inasadikika kuwa  Mzee Ambilikile Panja alizaliwa mwaka 1890 katika Kijiji cha  Kapelekeshi kilicho katika Kata ya Kafule wilaya Ileje.

Mzee Panja anasema hajui mwaka aliozaliwa na kwamba wakati ule walikuwa hawana kumbukumbu za tarehe mpaka shule za mkoloni zilipoanzishwa. Hivyo makadilio ya umri wake yanatokana na kumbukumbu ya matukio aliyoyashuhudia na kusimuliwa.

Mzee Ambilikile anakumbuka kipindi cha utumwa ambacho kilifanywa na Chifu Melele wa Wasangu miaka ya mwanzoni mwa mwaka 1900 kupitia kwa wakala wake ambaye anamkumbuka kwa jina la Tuta. Panja anasema kipindi hicho walikuwa wanajificha pamoja na Wazazi wao kwenye mapango ya mawe milimani. Alisema “ Tulikuwa tunajificha kwenye mapango na Wazazi wetu na Tuta alikuwa anatumia wenyeji wake kutuitwa kwa lugha ya Kindali ili tutoke lakini tulikuwa tunazuiliwa na wazazi tusiitike na wao walikuwa wanaogopa kuingia ndani, basi tulikaa ndani mpaka tukihakikisha wameondoka ndipo tulikuwa tunarudi nyumbani” .

Panja anakumbuka hadithi ya vita vya maji maji, anasema kuwa walikuwa wanasimuliwa kuwa vita inapiganwa kusini kati ya Wazungu na Waafrika ambapo waliambiwa Waafrika wana dawa ya kugeuza risasi kuwa maji. Wakati huo mzee Panja anasema alikuwa na ufahamu ila alikuwa hajaanza kuchunga kuchunga Ng’ombe kwa sababu baba yake hakuwa nazo.

Mzee Panja anakumbuka vita kuu ya dunia ya kwanza na alioa katika kipindi hicho mwaka 1916 ingawa anasema alioa kwa kuchelewa akijilinganisha na vijana wa umri wake.

Ukifuatilia tafiti zilizofanyika na Wataalam wa Anthropolojia kwa mfano; Wilson, M. ( 1963)  Good Company: A study of Nyakyusa Age – Villages. inaonesha kuwa Wanyakyusa  walikuwa wanoa kuanzia umri wa miaka 25. Wanyakyusa na Wandali wanafanana mila na desturi kwa kiasi kikubwa ikiwa ni pamoja na makuzi ya watoto wao kuanzia kufundishwa wajibu kwa jinsi na umri.

Kwa hiyo kama alioa mwaka 1916  akiwa na umri wa miaka 26 inawezekana alizaliwa mwaka 1990.

Pamoja na hayo mzee panja alioa Mke wa  Kwanza Mungajhoba Chufo ambaye alikuwa mke mdogo wa Chifu Mwambugha Musomba wa Kijiji cha  Malangali, Ileje lakini ndoa hiyo haikuchukua muda mrefu kwa sababu ilikuwa ilichukuliwa kama ni uporaji kiasi cha kumfanya apate adhabu ya kulipa faini kwa kosa hilo, mzee Panja hakubahatika kupata mtoto na Mke huyo. Baadaye alimwoa Agness Mlawa mwishoni mwa mwaka 1996 na wakajaliwa kupata watoto Marko Ambilikile na Kilonati na baada ya hapo alioa wake wengine wawili na kuweza kuzaa jumla ya watoto 24 kati ya hao 8 wa Kike na 16 wa Kiume. Mzee Panja ana Wajukuu 112 , Vitukuu na Vilembwe.

Mwaka 2014 mtoto wake wa Pili kwa mke  wa pili  Agness Mlawa alikuwa anaitwa Kilonati Ambilikile Panja  alifariki akiwa na umri wa miaka 98.

Aidha, alieleza kuwa kati ya watoto 24, ni watoto 11 tu walio hai mpaka anapotoa taarifa hiyo kwa msaada wa ukalimani wa mtoto wake Lawrance Ambilikile Panja Aprili 27,2017

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.