• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MWANGELA: WANANCHI WAPEWE ELIMU ZAIDI KUONGEZA HIFADHI YA KIMONDO

Posted on: November 28th, 2020

RC MWANGELA: WANANCHI WAPEWE ELIMU ZAIDI KUONGEZA  HIFADHI YA KIMONDO  

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Breg. Jen. Nicodemus Mwangela amewaagiza viongozi wa Wilaya ya Mbozi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi  juu ya faida ya kuongeza ukubwa wa eneo la hifadhi ya Kimondo lililopo kijiji cha ndolezi Kata ya Mlangali ambalo kwa sasa liko chini ya Mamlaka ya uhifadhi wa Ngorongoro.

Mkuu wa Mkoa ametoa agizo ilo alipokutana na Serikali ya Kijiji cha Ndolezi kufuatia baadhi ya wananchi kutoelewa vizuri mchakato wa fidia na faida ya kuongeza ukubwa wa eneo la Kimondo ambalo kwa sasa liko chini ya  Mamlaka ya uhifadhi wa Ngorongoro.

Serikali kupitia Mamlaka ya uhifadhi wa Ngorongoro ina mpango wa kuchukua Ardhi kwa fidia kwa baadhi ya wananchi wanaozunguka eneo la Kimondo kwa ajili ya kuleta wanyama mbalimbali pamoja na kuboresha miundombinu na kukifanya  Kimondo cha Mbozi kuwa eneo la utalii kwa Mkoa wa Songwe. 

Mkuu wa Mkoa amesema jambo ili ni la hiari linaitaji elimu zaidi na wananchi wakikubaliana kwa hiari basi serikali itakuja kufanya tathimini kwa kina na kila mtu atalipwa fidia yake kwa mujibu wa sharia na taratibu ndani ya miezi sita baada ya Serikali kufanya tathimini.

Pia, Mhe. Mwangela ametoa wito kwa wananchi ambao hawakubaliani na swala ili kwa sababu za kutokuwa na uelewa juu ya swala ili kutowatishia maisha au kuwaogopesha wale ambao wamekubali Ardhi yao ichukuliwe kwani jambo ili Serikali italifanya baada ya wananchi wote kukubaliana juu ya ili.

Bi. Celina Mwanda mkazi wa Ndolezi ambaye Ardhi iko eneo ambalo linahitajika na Ngorongoro ameiomba Serikali kuendelea kutoa elimu ya jinsi fidia itakavyolipwa kwenye mashamba pamoja na makazi ndio sababu kubwa ya baadhi ya wananchi wameshindwa kulipokea vizuri.

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. John Palingo amesema wamefanya mikutano na Serikali ya Kijiji pamoja na wananchi na kuwaeleza juu ya kuchukua ardhi yao kwa fidia kwa ajili kuongeza eneo la Kimondo na kuna baadhi ya wananchi wamekubali na kulipokea na wengine bado wamegoma kwa kuwa bado hawajaelewa vizuri.

Mbunge wa Jimbo la Vwawa, Mhe. Japhet Hasunga amesema kimondo hiki ni cha miaka mingi lakini hakikuwa na thamani lakini baada ya mimi kuteuliwa na Rais kwa nafasi ya Naibu waziri wa Utalii Serikali ilianza mchakato wa kukitangaza Kimondo cha Mbozi kwa kuleta pesa ya kujenga jengo la kisasa pamoja na kuanzisha siku ya Kimondo Duniani ambayo hufanyika mwishoni mwa mwezi Juni kila mwaka.

“Tusiwaze sana Kilimo sehemu ambazo kuna shughuli za utalii wananchi wanatengeneza pesa nzuri kuliko sisi tunaofanya Kilimo jambo ili la utalii liko vizuri tunachotaka ni taratibu za fidia zifuatwe” Mbunge wa Jimbo la Vwawa, Mhe. Japhet  Hasunga.

Mhe. Hasunga  amesema eneo ili Ngorongoro wakileta wanyama pamoja na kuliboresha vizuri litakuwa eneo nzuri kwa ajili ya kufanya utalii kwa Mkoa wa Songwe  na vijana wa kijiji cha ndolezi watapata ajila na kuboresha maisha yao.

Serikali ya Mkoa wa Songwe kwa kushirikiana na Mamlaka ya Uhifadhi wa Ngorongoro wanampango wa kukifanya Kimondo cha Mbozi na eneo ilo kuwa na vivutio mbalimbali vya utalii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.