• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI KUPIMA UPYA ENEO LA NANYALA KUTATUA MGOGORO.

Posted on: April 8th, 2022

SERIKALI KUPIMA UPYA ENEO LA NANYALA KUONDOA MGOGORO.

MBOZI: Serikali Mkoani Songwe imesema ina mpango wa kuligawa eneo la zaidi ya ekari 1,800 lenye hati namba 31 lililopo Kijiji cha Nanyala ambalo kwa muda mrefu limekuwa na mgogoro kati ya Kwanda cha Saruji cha Mbeya, wananchi wa Kijiji cha Nanyala pamoja na wadau wengine ambao wanafanya shughuli za uchimbaji madini katika kijiji hicho.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba amesema hayo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Aprili 8, 2022 na wananchi wa Kijiji cha Nanyala, Mbeya cement pamoja na wadau wanaofanya shughuli za uchimbaji katika Kijiji cha Nanyala.

Mhe. Mgumba amesema timu ya wataalamu iliyoundwa na Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan itapita kubaini maeneo yanayofaa kwa Kiwanda cha Mbeya Cement, kwa Kilimo, madini ya chokaa, marble na eneo la wananchi ili kila mtu abaki na eneo ambalo linafaa kwake kwa shughuli za kiuchumi.

Amesema kuna mgogoro  kwa sababu Serikali ilitoa hati ya miaka 99 ya kiwanja namba 31 kwa kiwanda cha Mbeya cement, wakati wapo wananchi wanaomiliki kisheria na wana hati za kimila, kuna wengine wameachiwa na babu zao pia kuna wadau wanafanya shughuli za uchimbaji wa madini na wamepewa leseni halali na Serikali ya Tanzania.

"Kiwanda cha Mbeya Cement kimeondoa kesi Mahakamani baada ya kuona hakuna masilahi ya kuendelea na kesi Mahakamani wakati wana uwezo wa kumaliza mgogoro huo kwa pamoja kati ya Mbeya Cement, wananchi wa Nanyala, wadau wanaofanya shughuli za uchimbaji na Serikali" Omary Mgumba.

Diwani wa Kata ya Nanyala, Mhe. George Musyani ameishukuru Serikali kuja na mpango wa kupima upya ardhi  kwani ndani ya ekari 1,800 ambazo Mbeya Cement wanadai ni za kwao na wananchi wa Nanyala wanalitegemea kiuchumi kwani wana mashamba yao, migodi na baadhi ya vitongoji vipo umo kama cha Majimoto, Iwanga, Udinde, Malema ambayo kuna miundombinu ya huduma za jamii.

Naye Julius Mwashilindi mwananchi wa Kijiji cha Nanyala amesema kitendo cha Mbeya Cement kuamua kumiliki ardhi bila ya kuwa na mkutano wa hadhara na kijiji ndio chanzo kikubwa cha mgogoro.

Aneth Gambi Mkazi wa Nanyala amesema ardhi ya Nanyala ni mali yao ambayo vizazi kwa vizazi vimeishi pale na wameiomba Serikali kutenda Haki.

Ikumbukwe kwa mara kadhaa wananchi wa Kijiji cha Nanyala wamelalamika kero yao hii kwa Waziri Mkuu pamoja na Rais wa Tanzania wa awamu ya 5 Mhe. Hayati John Magufuli alipofanya ziara 2019  Songwe na kuongea na wananchi wa Kijiji cha Nanyala.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.