• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA TAASISI ZA DINI KUTATUA CHANGAMOTO

Posted on: August 9th, 2022

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA TAASISI ZA DINI KUTATUA CHANGAMOTO

Na. Nicholaus Ndabila

SONGWE: Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Waziri Kindamba amesema Serikali itashirikiana na Taasisi za dini zote katika kutatua changamoto zilizopo ndani ya Mkoa wa Songwe.Mkuu wa Mkoa wa Songwe amesema hayo Agosti 4 alipowatembelea vongozi wa Parokia ya mtakatifu Patrick Vwawa pamoja na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kwa lengo la kujitambulisha kwa viongozi hao baada ya kuteuliwa na Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluh Hassan kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe.

Mkuu wa Mkoa amesema wakati Serikali inapita mitaani kuhakikisha ulinzi na usalama unakuwepo, viongozi wa dini wao wanasaidia kuweka amani kwenye mioyo ya watu kwani binadamu ni kiumbe mgumu sana akiachwa bila kupewa nasaha za kutosha basi amani na utulivu unakuwa mashakani.

“Kuna msemo unasema ukitaka kufanikiwa waweke viongozi wa dini karibu na ukitaka kufeli basi waweke viongozi wa dini mbali, Serikali tumechagua kuwaweka karibu viongozi wa Dini” Mhe. Waziri Kindamba.

Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Songwe ameomba ushirikiano kwa Taasisi za kidini kusaidia Serikali kutoa elimu kwa waumini wao juu ya kushiriki katika zoezi la SENSA ya watu litakalofanyika Agosti 23 pamoja kupata na kuhamasisha wananchi wapate chanjo ya UVIKO 19.

Mchungaji John Mwasakilali wa KKKT amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Waziri Kindamba kwa kuaminiwa tena na Rais wa Tanzania na kuletwa kwenye Mkoa ambao una mahitaji makubwa ya kimiundombinu na changamoto ili aweze kuzitatua.

Pia, Mch. Mwasakilali amemueleza changamoto kadhaa Mkuu wa Mkoa ambazo amemuomba kuzitafutia majawabu ikiwemo upungufu wa nishati ya kupikia katika mji wa Vwawa kama vile mkaa, kuni na bei kubwa ya gesi ya kupikia pamoja na upungufu wa maji katika mji wa Vwawa.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewaomba viongozi wa dini kutochoka kuishauri Serikali mara kwa mara ili kuweza kutatua changamoto kwa pamoja za wananchi na amewakaribisha ofisini kwake muda wowote watakapohitaji kufika.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.