• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SONGWE DC WAONGEZE NGUVU KUKAMILISHA UJENZI WA VITUO VYA AFYA

Posted on: July 16th, 2019

  Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemus Mwangela ameutaka Uongozi wa Wilaya ya Songwe Kuongeza jitihada na nguvu Zaidi katika kukamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Magamba na Mbuyuni pamoja na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya hiyo.

Brigedia Jenerali Mwangela ameyasema hayo leo mara baada ya kupokea taarifa ya mpango wa ukamilishaji wa miradi hiyo kutoka kwa uongozi wa Wilaya ya Songwe na kisha kuwapeleka katika Mradi uliokamilika wa Kituo cha Afya ya Isansa Wilaya ya Mbozi na ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili waweze kujifunza kwa vitendo.

“Baada ya kupokea taarifa yao ya ukamilishaji wa miradi ya ujenzi ya Wilaya ya Songwe, nimeona ni vema waje wajifunze kwa vitendo kwakuwa ukamilishaji wa miradi yao ya ujenzi umekuwa ukienda taratibu mno pia wajifunze kufanya kazi za serikali kwa teamwork”, amesisitiza Brigedia Mwangela.

Brigedia Jenerali Mwangela amesema miradi ya ujenzi ya Wilayani humo mingi bado haijakamilika na muda umewaishia hivyo kwa ziara hiyo wajifunze kuwa wenzao wamekalisha miradi hiyo  na inahudumia wananchi na pia kazi za serikali zinapaswa kukamilika kwa muda.

“Wao vituo vimechelewa sana kukamilika wamekuja wajifunze na waongeze nguvu ili waweze kukamilisha mapema, wameniambia wamejifunza kitu lakini pia wanapaswa kutambua kuwa kazi za serikali unapewa fedha, vifaa na muda maalumu wa kukamilisha”, ameeleza Brigedia Mwangela

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samuel Jeremia Opulukwa amesema wamejifunza kuwa wenzao wameweza kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya kwa viwango vizuri na wao watafanya hivyo ili wananchi waanze kupata huduma.

“Tumeona wenzetu wamekamilisha vizuri nasi tutajitahidi kukamilisha vizuri vituo vyetu ya Afya vya Magamba na Mbuyuni pamoja na hospitali ya Wilaya ili tuweze kutoa huduma kwa wananchi wetu ifikapo Julai 30, 2019”, amesema Opulukwa.

Naye Mganga Mkuu wa Wilaya ya Songwe Humphrey Masuki amesema wamejionea namna nzuri ya umaliziaji wa vituo vya Afya ili viwe na ubora na kutoa mfano kuwa wamejifunza namna nzuri ya upangaji makabati katika chumba cha kuhifadhi maiti na upangaji wa makabati na meza katika jengo la maabara.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.