• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SONGWE: WANANCHI WAHIMIZWA KUPIMA UKIMWI KUJUA HALI ZAO KUEPUKA MAAMBUKIZI MAPYA

Posted on: December 1st, 2020

 

SONGWE: WANANCHI WAHIMIZWA KUPIMA UKIMWI KUJUA HALI ZAO KUEPUKA MAAMBUKIZI MAPYA

Wananchi wa Mkoa wa Songwe wahimizwa kupima UKIMWI kujua hali zao za maambukizi hii inatokana na Mkoa kuwa na 86% ya watu wanaoishi na UKIMWI kufahamu hali zao wakati lengo la kitaifa tunatakiwa kufika 90% au zaidi watu kujua hali zao za maambukizi kwa wanaoishi na UKIMWI.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Breg. Jen. Nicodemus Mwangela amewataka watalamu wa Afya ifikapo Desemba 2021 kuhakikisha Mkoa uwe umetimiza lengo la 90% kwa kuwafikia wananchi wote ambao wanapaswa kujua hali zao za maambukizi ya UKIMWI.

Mkuu wa Mkoa ametoa agizo ilo katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani ambayo ufanyika kila Desemba mosi nas kwa Mkoa yamefanyika Wilaya ya Mbozi eneo la Ivungwa-Karasha na Hotuba ya Mkuu wa Mkoa kusomwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. John Palingo.

“Kwa kutofanya vizuri katika 90 ya kwanza kutapelekea watu wanaoishi na UKIMWI kutotambua hali zao hali ambayo itapelekea kuongezeka kwa maambukizi mapya katika jamii na kupunguza kasi ya kupambana na UKIMWI, kwani msimamo wa Mkoa wa Songwe ni kuwa Mkoa wa kwanza ifikapo 2030 kwa kumaliza kabisa maambukizi mapya ya UKIMWI, vifo vitokanavyo na UKIMWI na kutokomeza ubaguzi kwa walioathirika na UKIMWI huu utakuwa mchango wetu mkubwa kwa Tanzania” Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Breg. Jen. Nicodemus Mwangela.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dr. Hemed Nyembea amesema mikakati ya 90 tatu za kupambana na UKIMWI Songwe tunafanya vizuri kwenye 90 ya pili na tatu tub ado nguvu inatakiwa katika 90 ya kwanza, 90 ya kwanza watu wote wanaoishi na UKIMWI waweze kupima na kutambua hali zao, 90 ya pili wote waliopata UKIMWI kuanzishiwa dawa za kufubaza kwa 90 ya pili tumefika 96% na kwa 90 ya tatu inataka wote wanaoishi na UKIWMI wanaendelea kupata Dawa Songwe tumefika 95%.

Dr. Nyembea amesema Mkoa unaendelea na mkakati wa kupamba na UKIMWI kwa kuendelea kutoa ya huduma ya kupima kwa wananchi kwa kulengwa wale wenye sifa, kujikita kubaini watu wote wenye sifa ya kupimwa UKIMWI wanapokuja kwenye vituo vya kutolea Huduma pamoja na kuendeleza mkakati wa kufika lengo la 90 ya kwanza.

Mkazi wa Mbozi, Eliud Mwashambwa ameiomba Serikali kuendelea kuhamasisha watu wapime UKIMWI kupitia mikusanyiko mbalimbali inayokuwepo ili kuweza kutimiza lengo la 90% ya watu wanaoishi na UKIMWI kutambua hali zao.

Dr. Antony Galishi kutoka Worldvision Tanzania amesema shirika linaendelea kutoa elimu juu ya ukatili ya kijinsia na watoto katika makundi mbalimbali kwa kuwa ukatili nao umekuwa ni moja ya chanzo cha maambukizi mapya ya UKIMWI na lengo ni kuhakikisha ifikapo 2030 hakuna maambukizi mapya.

Mkoa wa Songwe una vituo vya Tiba ya Matunzo (CTC) 64 na vituo vya kukinga maabukizi ya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto 108.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.