• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA EBOLA

Posted on: August 19th, 2018

Wananchi wa Mkoa wa Songwe mna tahadharishwa juu ya uwepo wa ugonjwa wa Ebola uliotokea nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) katika jimbo la Kivu na kuenea mpaka katika jimbo la Ituri kuanzia Agosti 1, 2018.

Mpaka kufikia tarehe 15 Agosti, 2018 wagonjwa waliogundulika kuwa na virusi vya Ebola nchini DRC  walikuwa 51, wanaohisiwa 27 huku waliofariki wakiwa 44, kwa wastani kati ya watu 10 waliopata Ebola, watu 5 hadi 9 hufariki.

Tahadhari hii inatolewa kwasababu eneo la mpaka wa Tunduma hutumiwa na raia wa Congo kuingilia nchini Tanzania kupitia nchi jirani ya Zambia na hivyo ugonjwa huu kuwa hatarini kuingia nchini Tanzania licha ya kuwa Mkoa wa Songwe haujapakana na nchi ya DRC moja kwa moja.

Serikali ya Mkoa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeweka hali ya tahadhari na kuchukua hatua muhimu ili kuhakikisha ugonjwa huu hauingii nchini, naendapo utaingia uweze kuthibitiwa mapema.

Baadhi ya hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuwekwa huduma za uchunguzi eneo la Mpaka wa Tunduma, huduma za kulazwa na mahali pa maziko endapo watabainika wagonjwa wa Ebola na wengine kufariki.

Aidha mafunzo kwa watoa huduma za Afya yalitolewa, vifaa tiba/kinga na dawa vilinunuliwa na Mkoa unaendelea kufanya ufuatiliaji huku huduma ya uchunguzi kwa abiria wanaotumia mpaka wa Tunduma zikiendelea.

Virusi vya Ebola havienei kwa njia ya hewa bali huambukiza kwa njia Kuu Mbili, ambazo ni Kutoka kwa Wanyama kwenda kwa Watu (endapo utamgusa mnyama mwenye Ebola au kula nyama yake) na Kutoka kwa mtu mwenye Virusi vya Ebola kwenda kwa mtu mwingine (kwa kugusana, kugusa majimaji ya mwili au damu).

Dalili za kwanza za Ugonjwa wa Ebola zinafanana na za magonjwa mengine ambazo ni homa ya gafla, uchovu, maumivu ya koo, tumbo, misuli, kichwa na viungo vingine. Kwa dalili hizo, watu hufikiria kwamba wana magonjwa mengine kama vile malaria au homa ya matumbo.

Kwa kawaida hali inayofuata ni kichefuchefu na kuharisha pamoja na figo kutofanya kazi vizuri, huku wengine huanza kutokwa na damu kwenye matundu yote ya mwili kama pua, masikio, mdomoni na sehemu ya haja kubwa.

Wananchi mtambue ya kuwa mpaka sasa hakuna mgonjwa wa Ebola aliyegunduliwa nchini Tanzania, na mpaka sasa hakuna tiba maalumu ya ugonjwa wa Ebola isipokuwa mtu akipata huduma bora mapema kutoka kwa madaktari na wauguzi mara baada ya kugunduliwa na ugonjwa huu anaweza kuishi.

Pia kama kuna mtu ana dalili zilizotajwa hapo juu na ana historia ya kutembelea nchi jirani ya Congo, apelekwe haraka kituo cha tiba ili afanyiwe uchunguzi mapema.

Imetolewa Na;

Grace Gwamagobe

Afisa Habari

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

18 Agosti, 2018.

 

Kwa taarifa Zaidi tembelea tovuti ya mkoa wa Songwe www.songwe.go.tz katika kipengele cha matangazo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.