• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TANROADS KWA KUSHIRIKIANA NA WADAU KUURUDISHA MTO ZIRA KWENYE NJIA KUU, ENEO LA MBALA KANGA LIPITIKE MUD WOTE.

Posted on: August 12th, 2021

TANROADS KWA KUSHIRIKIANA NA WADAU KUURUDISHA MTO ZIRA KWENYE NJIA KUU, ENEO LA MBALA KANGA LIPITIKE MUD WOTE.

SONGWE: Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya ameiagiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kushirikiana na Mamlaka ya Bonde la Ziwa Rukwa kumaliza tatizo la kufurika na kuhama mto zira na kusababisha mawasiliano kati ya mji wa Mbalizi na Mkwajuni wilayani Songwe kukatika.

Kasekenya alitoa kauli hiyo wakati alipotembelea eneo hilo ambalo limekuwa linafurika Maji wakati wa masika na kusababisha mawasiliano kukatika ambapo Naibu Waziri huyo  alisema ili kumaliza tatizo la mto huo kuhamahama ni lazima mamlaka ya Bonde la ziwa Rukwa ishiriki ili kuweza kutoa mwongozo utakaosaidia kumaliza tatizo linalojitokeza Mara kwa Mara.

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Mhandisi, Msongwe Kasekenya (MB) amefanya ziara ya kutembelea Barabara ya Mbalizi-Mkwajuni katika eneo la Mbala-Kanga ambapo TANROADS Songwe wanajenga Box karavati 7 kwenye tuta la Barabara pamoja na kufika hadi eneo ambalo Mto Zira umeanza kuchepuka na kuacha Njia Kuu umbali wa kilometa 3.5 kutoka kwenye Daraja la Mto Ziara.

" Tutashirikiana na Bonde la Ziwa Rukwa ili waweze kutupa muongozo mzuri kwa sababu wao ndio wanahusika na maswala ya mito na maziwa lakini TANROADS itatoa utalamu wa namna ya kutengeneza Kingo" alisema na kuongeza.

"Kwa hali ilivyo hapa Mto Ziara ni lazima tutafute fedha kwa njia yeyote kwa kushirikiana na wadau wengine kama Mazingira, Wizara ya Mifugo, TAMISEMI ili tuweze kidhibiti hali hii" alisema Kasekenya.

Meneja wa TANROADS Mkoa wa Songwe, Mhandisi Yohana Kasaini alisema kutokana na mafuriko yaliyotokea  Serikali ilitoa Milioni 727 kwa ajili ya kujenga Box karavati 4 katika eneo la tuta la Barabara la Kanga-Mbala ambayo ni madaraja ya kudumu kwa ajili ya kuvusha maji ili lisiweze kubomolewa, lakini TANROADS Songwe imeweza kuongeza Box karavati 3 jumla kutakuwa na Box karavati 7 eneo la tuta la Barai la Kanga-Zira.

Mhandisi Kasaini alisema kwa ukarabati uliofanyika katika tuta la Kanga-Zira watakuwa wamefanikiwa maji yaweze kupita lakini ili kufanikiwa kwa 100% inatakiwa kazi ya kurudisha njia Kuu ya Mto Zira ifanyike kwa haraka ili maji yapite kwenye njia yake na TANROADS Songwe ifikapo mwishoni mwa Octoba  tutakuwa tumemaliza ujenzi wa boxi karavati 7 kabla ya Mvua haijaanza.

Mbunge wa Jimbo la Songwe, Mhe. Philip Mulugo amesema wananchi kutoka katika Kata 8 wamekuwa wakiathirika kukatika kwa mawasiliano kipindi cha Mvua katika eneo la Kanga-Zira na kusababisha kuwaongezea gharama ya maisha kwani iliwarazimu  kuzunguka hadi Mkoa wa Mbeya ili waweze kufika makao makuu ya Wilaya ya Songwe.

Aidha, Mulugo amemuomba Waziri Barabara ya Mbalizi-Mkwajuni hadi Patamela ichukuliwe kwa umhimu wake iweze kujengwa kwa kiwango cha lami ndani ya muda mfupi na amemuomba kufikisha kilio cha wana Songwe kwa Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuwasaidia.

Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Simon Simalenga amesema Songwe ni Wilaya ya kimkakati kiuchumi kwa Nyanda za Juu Kusini kutokaa na madini yanayochimbwa sasa, lakini sasa kuna madini ya Rare Earth  yataanza kuchimbwa Songwe, madini ambayo Duniani yanapatikana Nchi ya China na Tanzania tu, hivyo amemuomba Waziri kuweza kuitazama Barabara ya Mbalizi-Mkwajuni hadi Patamela kwa umhimu wake amewaomba viongozi wakuu wa Nchi, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais waweze kuwasaidia kupata Barabara ya Lami kwa sababu ya fursa za kiuchumi zilizopo Songwe za manufaa ya Mkoa na Taifa.

Aidha, Mkuu wa Wilaya amesema ofisi yake kwa kushirikiana na Mbunge wa Songwe, TANRROADS Songwe na wadau wote waliopo Songwe watashirikiana kuhakikisha wanahakikisha Mto Zira unarejea kwenye njia yake Kuu na lengo lake ni kuhakikisha ndani ya miezi 2 Mto Zira unarudi kwenye Njia Kuu yake.

Kwa kipindi cha miaka 2 mfululizo mawasiliano ya Barabara ya Mbalizi-Mkwajuni  kukatika katika eneo Kanga na Zira, juhudi mbalimbali za Viongozi wa Mkoa kwa kushirikiana na Mgodi wa SHANTA pamoja na TANROADS za kujaza kifusi kwenye tuta la Kanga na Zira na kutumia makontena zimekuwa na mbinu za muda mfupi na kufanya hali kujiridia mara kwa mara, lakini juhudi zinazofanywa sasa na TANROADS za kujenga boksi karavati 7 na Mpango wa kurudisha njia Kuu ya Mto Zira zinaonyesha zinaweza kuwa njia ya kudumu kwa watumiaji wa Barabara ya Mbalizi-Mkwajuni.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.