• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TANZANIA BADO YAKABILIWA NA UHABA WA DAMU SALAMATUNDUMA

Posted on: June 14th, 2022

TANZANIA BADO YAKABILIWA NA UHABA WA DAMU SALAMATUNDUMA: Tanzania haijafikia lengo la ukusanyaji wa damu salama kwa mujibu wa  Shirika la Afya Duniani linalopendekeza nchi kukusanywa idadi ya chupa za damu ambazo ni sawa na asilimia 1 ya idadi ya wananchi waliopo kwenye nchi au eneo hilo kwa wakati huo.Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Omary Mgumba  kwa niaba ya Waziri wa afya Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipokua mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya mchangia damu duniani ambayo kitaifa yamefanyika katika mji wa Tunduma mkoani Songwe.Mgumba amesema nchi ya Tanzania, inakadiriwa kuwa na wananchi milioni 55, inatakiwa kukusanya chupa za damu 550,000 ambayo ni sawa na asilimia 100 ya mahitaji ya nchi ikilinganishwa na idadi ya wananchi waliopo.“Takwimu za ukusanyaji damu, zimeonyesha kuwa na mafanikio ya kuongozeka kwa ukusanyaji damu mwaka hadi mwaka. Mwaka 2017/2018 jumla ya chupa za damu 257,557 ambayo ni sawa na 45% ya mahitaji zilikusanywa, kufanyiwa vipimo vya maabara, na kusambazwa. Idadi hii imeongezeka hadi kufikia chupa 312,714 sawa na 57% ya mahitaji kwa mwaka 2019/2020, na kufikia 331,279 ambayo ni sawa na 60% ya mahitaji ya nchi kwa mwaka 2020/2021 lakini bado ukusanyaji huu haijakidhi mahitaji”. Amesema Mgumba.Mkuu wa Mkoa huyo amesema pamoja na ongezezo hilo, bado nchi haijafikia malengo ya kukusanya chupa 550,000 ingawa chupa zilizokusanya mwaka 2022/2021 ni chupa 331,279 sawa na asilimia  sitini (60%), bado kuna pungufu ya chupa 218,721 sawa na 40%  ya mahitaji ya nchi.Mhe. Mgumba amesema bado kuna kazi ya kufanya ya kuhakikisha hilo pengo la asilimia 40 linazibwa ili kukidhi mahitaji ya damu na kuhakikisha kuwa wale wote ambao wanahitaji kuongezewa damu wanapata huduma hio kwa wakati, na kwa viwango na kiasi kinachohitajika.Aidha, ameomba ushiriki wa taasisi na vikundi mbalimbali katika kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuchangia damu ili kuweza kupunguza na hatimae kuondoa pengo lililobaki na kuondoa kabisa uhaba wa damu nchini.Maadhimisho ya siku ya mchangia damu duniani mwaka huu yamebebwa na kaulimbiu inayosema kuchangia damu ni kitendo cha mshikamano tuungane kuokoa Maisha.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.