• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TUNARUDI KWEYE MAZUNGUMZO NA JESHI-RC MWANGELA

Posted on: April 24th, 2019

  Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela amewataka wananchi wa Vijiji vya Itewe, Sasenga na Mboji Wilayani Mbozi kurejea katika Mazungumzo na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kufuatia Mgogoro wa mipaka ya ardhi.

Brig. Jen. (Mst) Mwangela ameyasema hayo alipotembelea vijiji hivyo akiambatana na uongozi wa Kambi ya Jeshi ya Kikosi cha KJ 845 ambao wamekuwa kwenye mgogoro wa mipaka na vijiji hivyo tangu mwaka 1979.

Amesema kuwa eneo ambalo linatambulika rasmi kuwa linamilikiwa na Jeshi lina ukubwa wa hekta 1398 na hivyo mwananchi yoyote hataruhusiwa kumiliki eneo hilo na endapo yupo ambaye anaishi katika eneo hilo atoke, aidha Jeshi liliomba eneo lingine ambalo ndilo lina mgogoro.

“Tunarudi kwenye mazungumzo, Jeshi na vijiji vyote vya Itewe, Sasenga na Mboji, ninacho waomba, kila upande ulete uthibitisho wa umiliki wa eneo lake, mkisha wasilisha hati zenu au hata vithibitisho vya umiliki wa maeneo yenu tutakaa tujadiliane ili mgogoro huu uishe kwa amani”, amesisitiza Brig. Jen. (Mst) Mwangela

Aidha Brig. Jen. (Mst) Mwangela amewataka wananchi wa vijiji vyenye Mgogoro na Jeshi kuendeleza amani na kukubali kumaliza mgogoro huo kwa njia ya majadiliano, pia watambue kuwa Jeshi lipo kwa ajili ya wananchi hao.

“Mimi sitaegemea upande wowote katika mgogoro huu kwani natambua wananchi ni muhimu na jeshi pia ni taasisi ambayo ni muhimu Mkoani Kwetu kwa ajili ya ulinzi na usalama wetu, hivyo basi itakapo bainika jeshi linahitaji eneo zaidi basi wananchi wenzangu tuwafikirie hawa lakini pia tutahakikisha wananchi wanaondoka kwa utaratibu mzuri”, ameongeza Brig. Jen. (Mst) Mwangela.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Sasenga Yaledy Hassan Wegga amesema wananchi wako tayari kutoa eneo kwa Jeshi endapo utaratibu mzuri utafuatwa kwani wanatambua umuhimu wa Jeshi kwa ajili ya ulinzi na usalama wa raia na mali zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA MOMBA KUJADILI HOJA ZA CAG

    June 11, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI HOJA ZILIZO BAINISHWA KATIKA RIPOTI YA CAG HALMASHAURI YA MBOZI

    June 10, 2025
  • RC CHONGOLO APIONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE KWA KUPATA HATI SAFI

    June 10, 2025
  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.