• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WADAU WATAKA RASILIMALI ZIGAWIE VIZURI KUPATA MATOKEO MAZURI YA WATOTO.

Posted on: September 8th, 2022

WADAU WATAKA RASILIMALI ZIGAWIE VIZURI KUPATA MATOKEO MAZURI YA WATOTO.

SONGWE: Wadau wa maendeleo wametoa wito kwa Taasisi mbalimbali na Serikali kugawa Rasilimali vizuri kwa watoto ili matokeo chanya yapatikane.

Witu huo umetolewa kwenye Jukwaa la juu la kujadili changamoto, fursa na sera lililofanyika kwa mara ya kwanza Tanzania katika Mkoa wa Songwe 8 Septemba 2022.

Mwakilishi wa UNICEF Tanzania, Shalini Bahumuna amesema wadau tumekusanyika hapa ili kujifunza jinsi tunavyotekeleza sera kwa kugawanya vizuri Rasilimali na kupata matokeo bora kwa watoto, Wanawake na familia zao.

Shalini Bahumuna amesema ni swala la kutumia Takwimu zetu vizuri na kufanya maamuzi sahihi kwa kutumia Rasilimali chache zilizopo na kuboresha matokeo katika sekta za kijamii kama Elimu na Aya.

"UNICEF hatuwezi kufanya pekeyetu ni lazima sote tushirikiane ndio maana leo zipo Wizara za kisekta kama OR TAMISEMI, Elimu, Fedha na Mipango pamoja na wadau wengine wa maendeleo wa ndani na nje ya Nchi" Shalini Bahumuna Mwakilishi wa UNICEF Tanzania.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Songwe, Ndg. Elynico Mkola amesema watoto wenyewe ndio waanzilishi wa harakati za kudai elimu na haki zao miaka ya 1970 Soweto Nchini Afrika Kusini sisi kama wazazi na walezi tuna deni kubwa la kuwasaidia sasa.

"Chama kitasaidia kuwaeleza wananchi kuhusu mambo yote ambayo wamekubaliana kwenye kikao cha wadau" Ndg. Elynico Mkola.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Waziri Kindamba amesema pamoja Songwe inazalisha sana chakula lakini bado kuna tatizo la udumavu kwa watoto wa umri chini ya miaka 5 kwa 43% ukilinganisha na wastani wa kitaifa wa 32%.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Juma Homera amezishauri Halmashauri kutenga Bajeti kwa ajili ya kusaidiana na wadau katika kuboresha elimu kwa kutoa mafunzo kwa waalimu na kutatua upungufu wa waalimu.

Mhe. Juma Homera amezitaka Halmashauri kutotegemea kila kitu kifanywe na Serikali kuu, kwani Serikali kuu imejenga miundombinu mingi ya Elimu pamoja na kulipa mishahara ya watumishi.

Halmashauri lazima ziwe na mkakati wa kuweka Bajeti katika sekta ya Elimu kwa ajili ya kupata waalimu wa muda mfupi ambao wapo mtaani na wamehitimu vizuri, hii itamsaidia sana Mhe. Samia Suluh Hassan Rais wa Tanzania katika kutatua changamoto kwa wananchi wake.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.