• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAFUNGWA 96 MKOANI SONGWE WAPATA MSAMAHA WA RAIS

Posted on: December 10th, 2019

  Wafungwa 96 Mkoani Songwe wamekuwa miongoni mwa wafungwa Zaidi ya 5000 waliopatiwa msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kufuatia maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika yaliyofanyika jana jijini Mwanza.

Mapema leo Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela amefika katika gereza la Mbozi ambapo wafungwa 45 wanapatiwa msamaha wa Rais huku wafungwa wengine wakiwa katika Magereza ya Wilaya za Ileje na Songwe ambapo amezungumza na wafungwa hao kabla hawapewa ruhusa ya kuondoka gerezani hapo.

“Nimeingia gerezani na kukuta wafungwa waliopata msamaha wa Rais Magufuli wakiwa na furaha na wamempongeza sana Rais wetu, lakini pia wafungwa waliobaki wamefurahia uamuzi wa Rais Magufuli wa kutoa msamaha kwani na wao wana tumaini la kupatiwa msamaha siku za baadae.”, amesema Brig. Jen. Mwangela.

Brig. Jen. Mwangela ameongeza kuwa wafungwa waliobaki wamempa changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na matatizo ya uhaba wa maji na ucheleweshaji wa nakala za hukumu mambo ambayo ameahidi kuyashughulikia haraka iwezekanavyo.

Kamishna Msaidizi wa Magereza Laizack Mfaume Mwaseba amesema amekuwa akipokea malalamiko ya ucheleweshaji wa nakala za hukumu kutoka kwa wafungwa na amekuwa akiwasiliana na mahakimu ili waweze kuzitoa nakala hizo kwakuwa ucheleweshaji huo unawanyima haki wafungwa ya kukata rufaa.

Ameongeza kuwa pamoja na changamoto ya maji katika gereza hilo kuna changamaoto za uhaba wa vitendea kazi na sare kwa wafungwa mambo ambayo tayari wamesha yawasilisha kwa kamishana Mkuu wa Magereza kwa ajili ya utatuzi.

Mmoja wa wafungwa wa gereza la Mbozi Victoria Adam amemshukuru Rais Magufuli kwa msamaha alio mpatia na kumuombea kwa Mungu aendelee kumlinda huku akieleza kuwa amejifunza mambo mengi alipokuwa gerezani na sasa anaenda kuwa raia mwema.

Naye Fred Andrea Daud ambaye amepata msamaha wa Rais Maguufuli amesema bahati aliyoipata ya Msamaha ataitumia vizuri kwa kufanya kazi halali kwakuwa Vijana wengi wamekuwa wakichagua kazi ambazo zinawaingiza katika matatizo

Ameongeza kuwa magereza ni sehemu ya urekebishaji na yeye amerekebika hivyo anawashauri vijana wote wafanye kazi halali ambazo hazitawaletea matataizo kwakuwa kazi halali zipo nyingi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.