• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAKULIMA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA KIWANDA CHA KUCHAKATA PARACHICHI

Posted on: July 16th, 2022

WAKULIMA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA KIWANDA CHA KUCHAKATA PARACHICHI

SONGWE: Kiwanda cha kuchakata parachichi cha Lima kilichopo wilayani Mbozi kina malengo ya kufikia kuchakata maparachichi tani 100 kwa siku kwa ajili ya kupata mafuta yanayofaa kwa matumzi ya vipodozi kutoka tani 48 ya sasa.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa kampuni ya Lima, Ndg. Tinson Tuloline Nzunda wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe alipotembelea kiwandani hapo tarehe 14 Julai 2022 kujionea jinsi kazi zinavyoenda.

Tinson Nzunda amesema tangu kiwanda kianze kufanya kazi Juni 2021 tani 2,700 za matunda ya parachichi zimeishachakatwa na kupata tani 231 za mafuta yanayofaa kwa vipodozi.

“Kampuni kwa sasa tunafunga mitambo mingine mikubwa na lengo letu ni kuweza kuchakata parachichi tani 100 kwa siku na kwa mwaka itakuwa zaidi ya tani 36,000 hivyo wakulima wachangamkie fursa ya kulima parachichi” Tinson Nzunda Mkurugenzi wa Lima.

Pia, Ndg. Nzunda amesema kwa sasa wanalazimika kuagiza maparachichi kutoka Mkoa wa Kagera, Kigoma na Kilimanjaro kwa ajili ya mahitaji ya kiwanda, hii ni kwa sababu maparachichi ni zao la msimu hivyo inapotokea sio msimu wake tunalazimika kwenda kuagiza kwingine ingawa ata ambayo yanakuwepo wakati wa msimu bado hayatoshelezi mahitaji ya kiwanda.

Parachichi la kisasa lina kiwango kikubwa cha mafuta ambayo tunayahitaji tofauti na haya maparachichi ya zamani au ya mbegu ya asili hivyo tunawaimiza wakulima kulima parachichi la mbegu ya kisasa amesema, Ndg. Tinson Nzunda.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Omary Mgumba amesema uhaba wa parachichi kwenye kiwanda cha Lima ni fursa kubwa sana kwa wananchi wa Songwe kuanza kuwekeza kwenye parachichi kwa kuwa kuna uhakika wa soko.

“Miaka ya nyuma wakulima walianza kukata miti ya maparachichi kwa kuwa walikuwa hawana uhakika wa soko lakini uwepo wa kiwanda cha kuchakata parachichi ndani ya Songwe ni fursa tena kwa wakulima kuanza kuwekeza tena kwani soko lipo na la uhakika” Mhe. Omary Mgumba.

Serikali tumelichukua na tunakwenda kuhamasisha kilimo cha parachichi ambacho itakuwa ni faida kwentu Serikali tutaweza kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja, tutatunza mazingira kwa kupanda miti kwa kuwa parachichi ni zao la miti lakini jambo la pili tutaongeza malighafi ya kiwanda hiki.

Kwa upande Mkuu wa wilaya ya Mbozi, Mhe. Cosmas Nshenye amemshukuru mkurugenzi wa Lima Ndg. Tinson Nzunda kwa kuwekeza nyumbani kwao na kutengeneza ajira za kutosha.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa amesema Serikali inaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme ambao hautakuwa changamoto kwa wawekezaji wa viwanda, kituo kikubwa kinajengwa Tunduma cha zaidi ya KV 440 ambacho kikikamilika kitatatua changamoto ya upungufu wa umeme kwenye viwanda vya Mkoa wa Songwe.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.