• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI ELFU 13 KUPATA HUDUMA ZA UPASUAJI

Posted on: September 12th, 2018

  Wananchi 13,476 wa kata ya Kapele yenye vijiji nane na vitongoji 39 Wilayani Momba, wanatarajia kupata huduma za upasuaji ikiwemo upasuaji wa dharura kwa akina mama wajawazito kufuatia kuanza kwa ujenzi wa kituo cha Afya katika kata hiyo.

Wananchi hao waliojitokeza kwa wingi na kujitolea nguvu kazi kwa kusafisha eneo la ujenzi na kuchimba msingi wamesema, kukosekana kwa kituo cha Afya katika kata hiyo kulipelekea wao kufuata huduma za upasuaji takribani kilomita 106 huku miundombinu ya barabara ikiwa mibovu.

Wamesema wanaishukuru serikali kwa kutoa shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho kinachotarajiwa kukamilika ifikapo Disemba 2018 na hivyo kuwapunguzia gharama za usafiri wa kufuata huduma hizo mbali.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Kapele Erasto Simchimba amesema kazi zilizokwisha fanyika katika eneo la ujenzi ni upimaji wa eneo hilo la ekari 25, kukusanya mawe na mchanga na uagizaji wa vifaa vya ujenzi huku hamasa ya wananchi kujitolea ikiwa ni kubwa.

Simchimba amesema, “wananchi wamehamasika kujitolea kwakuwa wanafahamu umuhimu wa kituo hiki na tayari wamefyeka miti na kusawazisha eneo hili na sasa wanachimba msingi wa majengo matano ambayo ni jengo la wagonjwa wa nje, jengo la wagonjwa wa ndani, chumba cha upasuaji, maabara na jengo la wazazi”.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemus E Mwangela ametembelea eneo la ujenzi wa Kituo cha Afya Kapele na kushiriki pamoja na wananchi shughuli ya uchimbaji wa msingi wa kituo hicho.

Brig. Jen. Mwangela amewasisitiza wananchi kuendelea na moyo huo wa kujitolea kwakuwa kituo hicho cha afya kitawanufaisha wao huku akiwasisitiza kutunza miundombinu ya kituo hicho mara kitakapokamilika.

Aidha kuhusu ubovu wa barabara ya Kakozi-Ilonga yenye urefu wa Kilomita 50 amewaeleza wananchi hao kuwa anawapongeza Wakala wa Barabara Vijijini katika Halmashauri ya Wilaya ya Momba kwa kutenga shilingi milioni 300 ambazo zitaanza matengenezo kwa kilomita 18 za barabara hiyo.

Wakati huo Brig. Jen. Mwangela amewataka wananchi wa kata ya Kapela ambayo iko mpakani na nchi jirani ya Zambia kuchukua tahadhari ya ugonjwa ebola na kutoa taarifa katika zahanati iliyopo katika kata hiyo mara watakapomuhisi mtu mwenye dalili za ugonjwa huo.

Ameongeza kuwa kata ya Kapele iko mpakani na kumekuwa na mwingiliano na nchi jirani ya Zambia kutokana na mahusiano mazuri hivyo kuwa katika hatari ya kupata ugonjwa huo kutoka kwa raia wa Congo wanaopitia Zambia aidha amewasihi kudumisha mahusiano mazuri kwa kutii sheria za nchi jhiyo wanapokuwa huko.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA MOMBA KUJADILI HOJA ZA CAG

    June 11, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI HOJA ZILIZO BAINISHWA KATIKA RIPOTI YA CAG HALMASHAURI YA MBOZI

    June 10, 2025
  • RC CHONGOLO APIONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE KWA KUPATA HATI SAFI

    June 10, 2025
  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.