• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANUFAIKA WA TASAF WAMEWEZA KUPIGA HATUA

Posted on: March 1st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig.Jen. (Mst) Nicodemus E Mwangela amefanya ziara ya kukagua  utekelezaji wa Mpango wa TASAF katika Wilaya za Momba na Ileje ambapo amesema ameridhishwa na namna ambavyo wanufaika wa mpango huo wameweza kupiga hatua katika kujikwamua kutoka katika umasikini.
Brig.Jen. (Mst) Mwangela amewashauri wanufaika hao kuendelea kuwekeza katika elimu na afya kwani ndio msingi mkubwa wa kujiondoa kwenye umasikini.
"Ndugu zangu hakuna mtu aliyezaliwa ili awe masikini, wote tunaweza kutoka kwenye umasikini endapo tutahakikisha tunawasimamia watoto wetu walioko kwenye mpango wa TASAF wapate elimu pia tuwekeze katika afya hasa kwenye mfuko wa afya ya jamii ili tuweze kupata huduma za afya", Brig.Jen. (Mst) Mwangela.
Brig.Jen. (Mst) Mwangela pia amewasisitiza kutowakatisha masomo watoto walioko kwenye mpango wa TASAF kwa kuwaozesha mapema bali wawasimamie watoto hao hususan wa kike wasome mpaka watakapo hitimu ili waweze kuwakomboa wazazi wao na wajikomboe wenyewe kutoka katika umasikini.
Ameongeza kuwa lengo la mfuko wa TASAF ni kumsaidia mnufaika apige hatua haraka kutoka kwenye umasikini na aweze kuyamudu maisha ya kaya yake kwa kuwa na uhakika wa chakula, huduma za fya na elimu na hata kuchangia katika pato la Taifa kwa kuzalisha mali kupitia kilimo, ufugaji na biashara.
Jakson Mwabeza mmoja wa wanufaika kutoa Wilaya ya Ileje kijiji cha Ilulu amesema kabla ya kuingia katika mpango wa TASAF maisha yake yalikuwa duni lakini baada ya mpango huo ameweza kujenga nyumba ya bati, amenunua baiskeli 14 na ana uhakika wa chakula nyumbani.
"Wakati mkutano wa kijiji umeitishwa ili kuwapata walengwa wa TASAF nilionekana mimi pia ni mmoja wapo wa walengwa ila niliona kama udhalilishaji kutokana na hali yangu ya umasikini, nashukuru mtendaji wa kijiji kwa kunielewesha kuhusu mpango huu, hadi sasa mafanikio niliyo nayo yametokana na mpango wa TASAF", amesema Mwabeza.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.