• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WARATIBU ELIMU WAZEMBE KUCHUKULIWA HATUA KALI MKOANI SONGWE

Posted on: December 6th, 2019

   Waratibu Elimu kata na Wasimamizi wa Sekta ya Elimu Mkoa wa Songwe waliobainishwa katika ripoti ya uchunguzi wa hali ya sekta ya Elimu kuwa ni wazembe katika kusimamia maendeleo ya elimu watachukuliwa hatua kali za kinidhamu.

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila amesema hayo jana wakati wa kikao na Waratibu Elimu Kata na Maafisa Elimu ili kutathmini maendeleo ya Sekta ya Elimu kwa mwaka 2019 na kupanga mikakati ya kuboresha elimu kwa mwaka 2020.

“Tuliwapa kazi wadhibiti ubora ya kufanya uchunguzi kwanini Mkoa wetu haufanyi vizuri kielimu na ripoti yao imebainisha uwepo wa uzembe wa waratibu elimu Kata katika usimamizi, sasa nitachukua hatua kali kwa waratibu elimu wote wazembe.”, amesema Kafulila.

Kafulila amesema Waratibu Elimu kata wote walisaini Mkataba ambao uliwataka kusimamia Sekta ya elimu na kuhakikisha kiwango cha elimu kinapanda lakini pia serikali imewawezesha posho na usafiri lakini wapo baadhi yao ambao wameshindwa kutekeleza majukumu yao.

“Serikali imewapa posho na Waratibu Elimu Kata lakini baadhi yao wamebainishwa katika ripoti kuwa wanafanya kazi kwa kuogopana na kuendekeza urafiki, hawawachukulii hatua walimu na wakuu wa shule ambao hawatimizi majukumu yao, hao hatuwezi kuwavumilia.”, amesisitiza Kafulila.

Naye Mwenyekiti wa Wadhibiti Ubora wa Elimu Mkoa wa Songwe Mwalimu Jackson Lwafu amesema walitathmini kwanini baadhi ya shule katika Mkoa wa Songwe zimeshuka kielimu na walibaini kuwa usimamizi dhaifu umechangia kwa kiasi kikubwa.

Lwafu amesema endapo wasimamizi wa Elimu Mkoa wa Songwe watatambua majukumu yao na kuyasimamia, maendeleo ya sekta ya Elimu Mkoa wa Songwe yatakuwa mazuri.

Mratibu Elimu Kata ya Mkukwe Wilayani Songwe Mwalimu Judith Mwasoke amesema taarifa ya wathibiti ubora inasikitisha kwakuwa ili kuwe na mafanikio lazima taratibu zifuatwe hivyo suala la kuoneana aibu na kuogopana halifai na waratibu Elimu Kata wenye tabia hiyo waache.

Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma Mtafya Wilson amesema kwa mwaka 2020 watahakikisha walimu wanafundisha vipindi vyote pamoja na kuwasimamia Waratibu Elimu Kata wanatimiza wajibu wao.

Afisa Elimu Mkoa wa Songwe Juma Japhet Kaponda amesema Matokeo ya darasa la saba mwaka 2019 hali haikuwa nzuri kwakuwa Mkoa ulipanda ufaulu kwa asilimia 1.65 kwa kuwa na ufaulu wa asilimia 75 na Mkoa ukishika nafasi ya 21 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2018 wa asilimia 73 na nafasi ya Mkoa wa Songwe ilikuwa 17.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA MOMBA KUJADILI HOJA ZA CAG

    June 11, 2025
  • RC CHONGOLO AONGOZA KIKAO CHA KUJADILI HOJA ZILIZO BAINISHWA KATIKA RIPOTI YA CAG HALMASHAURI YA MBOZI

    June 10, 2025
  • RC CHONGOLO APIONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE KWA KUPATA HATI SAFI

    June 10, 2025
  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.