• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJIRI KWENYE UZINDUZI WA SOKO LA MADINI MKOANI SONGWE

Posted on: May 9th, 2019

  Soko la madini Mkoani Songwe litakuwa Wilayani Songwe na tunaamini ya kwamba wale waliozoea biashara za ujanja ujanja watakasirika, watabeza na kuhujumu lakini Kamati ya Usalama Wilaya ya Songwe imejipanga kuhakikisha hili litakamilika- DC Songwe Samuel Jeremia

Baada ya tarehe 8 Mei, 2019 yeyote atayeuza madini mkoani Songwe nje ya Soko la madini la Mkoa anatenda kosa la jinai na adhabu yake ni kutaifishwa mali, kufunga mwaka mmoja au vyote viwili kwahiyo nina watahadharisha tufuate sheria Pia Kamati ya Usalama Wilaya tutaanza kufanya ukaguzi na yeyote atayekamatwa atachukuliwa hatua za kisheria- DC Songwe Samuel Jeremia

Kila siku kutakuwa na Kilogramu tatu za dhahabu ambazo zitaleta mauzo ya shilingi milioni 270 na kwa mwezi itakuwa bilioni 6.7, fedha ya serikali itakuwa milioni 472 na halmashauri ni milioni 20.2 kwa mwezi ambapo fedha hizi zilikuwa hazipatikani kabisa- DC Songwe Samuel Jeremia.

Soko hili la madini litawasadia hasa wachimbachi wadogo kutambulika na kuzuia utoroshaji wa madini tuna Imani tatizo la kudhulumiana na kupunjana litakwisha hivyo nawasihi wote wanaohusika na sekta ya madini kulitumia- RC Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela.

Nawapongeza uongozi na wanachama wote wa chama cha wachimbaji wadogo kwa kuonyesha nia na kukubali kulipokea soko hili madini, mmeonyesha uzalendo na sisi tutashirikiana nanyi, kwani tunatambua kuwa soko hili ni kiunganishi kati ya wauzaji na wachimbaji RC Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela.

Mkoa wa Songwe una leseni 24 za utafiti wa madini, 101 uchimbaji mdogo, 5 za wachimbaji wa kati na kwa mwezi Machi Wilaya ya Songwe ilizalisha kilogramu za dhahabu 411.1- RC Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela.

Umuhimu wa soko la madini utakuwa ni uwepo wa soko la uhakika la madini ambalo litakuwa na malipo halali, soko litaondoa tatizo la kudhulumiwa na kupunjwa, Uwezekano wa kuibiwa hautakuwepo, Bei itaratibiwa na serikali na hiyvo kumnufaisha muuzaji na mnunuzi na litawezesha uwepo wa takwimu za uhakika- RC Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela.

Nawaelekeza Tume ya Madini na Wakala wa Vipimo kuhakikisha wanasimamia vifaa na taratibu zitakazotumika katika kupima madini hayo ili kuepuka malalamiko RC Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela.

Katibu wa Chama cha wachimbaji wadogo (SOREFA) Mkoani Songwe Elias Pangani amesema wachimbaji wadogo wako radhi na ni walipaji wazuri wa Kodi ya Serikali, wanaipongeza serikali kwa kuanzisha soko la madini kwani wamekuwa wakihangaika kutafuta masoko ya uhakika.

Kuzalisha kitu bila ya uwepo wa masoko ya uhakika ni kazi ngumu, kwahiyo wazo la uanzishwaji wa masoko ya madini ni jambo la kuungwa mkono, tunampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli ambaye ndiye muasisi wa wazo hili, nasisi kama Mamlaka ya Mapato Nchini tunaahidi na tuko tayari kutoa ushirikiano- Naibu Kamishna Mkuu Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) Msafiri Mbibo

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.