• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ZAHANATI YA NJELENJE KUANZA KUTOA HUDUMA

Posted on: May 18th, 2023

ZAHANATI YA NJELENJE KUANZA KUTOA HUDUMA JUNI 2023.

SONGWE: Wananchi wa kitongoji cha Njelenje kilichopo kijiji cha Mbangala Kata ya Mbangala Halmashauri ya Wilaya ya Songwe pamoja na maeneo jirani ya kibaoni, mteka, kwa yanga, nzega na kasisi kuanza kunufaika na huduma za Afya ifikapo Juni 2023 baada ya Zahanati yao kukamilika kwa 100%.

Akimuwakilisha Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Songwe, Ephrem Mgimba amesema Serikali ya awamu sita imetoa fedha Milioni 50 za ukamilishaji wa Boma la Zahanati ya Njelenje baada ya wananchi wa Njelenje kwa nguvu zao walifanikiwa kujenga Boma la thamani ya milioni 14.

Ephrem Mgimba ametaja huduma ambazo zitaanza kutolewa ni kliniki kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano, kujifungua kwa njia ya kawaida na huduma za matibabu kwa wagonjwa wa nje.

Kuzenza Magolanga mwananchi wa kitongoji cha Njelenje amesema anafuraha kuona Serikali inawasogezea huduma ya Afya kwani hadi sasa wanatumia shilingi 40,000 za usafiri wa pikipiki kufuata huduma za Afya makao makuu ya Kijiji chao cha Mbangala na Wilayani Mkwajuni.

Benson Lyanga mkazi wa kitongoji cha Njelenje ametoa wito kwa Serikali kuharakiaha kuwapeleka watalamu wa Afya katika Zahanati ya Njelenje ili waweze kuokoa maisha ya wananchi wa Njelenje.

Akitoa majibu ya Serikali, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe, Ndg. Vanscar Kulanga amesema huduma za matibabu zitaanza ifikapo Juni 2023 ili kufanikisha lengo la Serikali kwa wananchi wa Njelenje.

"Hapa tunataka ifikapo Juni 2023 muanze kutibiwa, muwakute watalamu, mzikute Dawa, mama wajawazito waanze kujifungulia hapa kwa usalama" Ndg. Vanscar Kulanga Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe.

Aidha, Ndg. Vanscar Kulanga amewapongeza wananchi wa Njelenje kwa moyo wao wa kujitolea nguvu kazi za thamani ya milioni 14 walizotumia kuinua Boma la Zahanati na kumuomba Mwenyekiti wa kijiji kuendelea na moyo huo kwenye miradi mbalimbali ambayo italetwa na Serikali.

MWISHO.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZINDUZI WA PROGRAM JUMUISHI YA TAIFA YA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO (PJT-MMMAM) MKOA WA SONGWE

    September 21, 2023
  • UZINDUZI WA CHANJO YA POLIO MKOA WA SONGWE 2023

    September 21, 2023
  • MKUTANO WA SITA (6) WA BARAZA LA BIASHARA 2023

    September 13, 2023
  • ZIARA YA SIKU TATU YA WAZIRI WA AFYA MHE. UMMY MWALIMU MKOA WA SONGWE

    September 11, 2023
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.